Tangazo

April 25, 2016

Airtel yakabidhi hundi ya Milioni 11 kwa Mfuko wa Mawasiliano kwa Watu (UCAF)


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Bi. Beatrice Singano Mallya (kushoto) akimkabidhi  hundi ya shilingi milioni 11 katibu wa mfuko wa mawasiliano kwa watu Justina Mashiba kwa ajili ya mashindano ya ICT kwa wasichana wa kidato cha tatu. yaliyoandaliwa na UCAF ( Universal Communications Services Access Funds ) na kushirikisha wasichana 240 hapa nchini, na kupata washindi sita watakaoenda kushiriki nchini Ethiopia mwishoni mwa mwezi huu, Airtel ni mdhamini wa mashindano hayo. Hafla hiyo ya makabidhiano ilifanyika  katika ofisi za makao makuu ya Airtel jijini Dar Es Salaam.
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

· Wasichana sita kwenda kushiriki mashindano ya ICT nchini Ethiopia

DAR ES SALAAM

Airtel yakabidi hundi ya shilingi millioni 11 kwa mfuko wa mawasiliano kwa watu (UCAF) kama wadhamini wa mashindano ya ICT kwa wasichana wa kidato cha tatu, yaliyoandaliwa na UCAF (Universal Communications Services Access Funds ) na kushirikisha wasichana 240 hapa nchini, na kupata washindi sita mwanzoni mwa mwezi huu na kutarajiwa kuondoka kuelekea  nchini Ethiopia mwishoni mwa mwezi huu  na kushiriki mashindano ya mwisho.

Akizungumza wakati wa makabidhiano yaliyofanyika  katika  ofisi za makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam,  Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Bi. Beatrice Singano Mallya  alisema “kama sehemu ya kusaidia jamii ambayo tunafanya biashara, Airtel Tanzania imeendeleza dhamira yake ya  kusaidia  vijana hapa nchini kwa njia mbali mbali. Udhamini huu utawasaidia mabinti hawa katika safari yao kuelekea nchini Ethiopia katika ngazi nyingine ya juu ya mashindano haya.

Mallya  aliendelea kusema kuwa kuwainua vijana hawa ni sawa na kuinua taifa letu la kesho. Kwani ujuzi waliokuwa nao si mdogo hivyo inatupa faraja kubwa hasa sisi wamama kuona kwamba wamama wa taifa la kesho nao wapo mstari wa mbele katika taaluma ya ICT”.

Akipokea hundi hiyo nae  katibu wa mfuko wa mawasiliano kwa watu, Justina Mashiba alisema " Tunaishukuru kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel kwa kutuwezesha kufanikisha mashindano haya  na vile vile kuwawezesha vijana hawa kuweza kufikia ndoto zao.Hii inaonyesha dhamira ya dhati ya Airtel ya kuinua vijana hapa nchini na kuwawezesha kufikia ndoto zao”.

 Airtel imejipanga katika kuinua vijana hapa nchini katika sekta mbali mbali  kuhakikisha kwamba vijana wanainuliwa na kuweza kuendesha maisha yenye matumaini na faraja tele. Ni makusudio yetu kuendeleza jitihada hizi za kuhamasisha mazingira ya ICT hapa Tanzania. Aliongeza, “Tunaamini katika uwezo wa ICT  kuwawezesha vijana kutimiza malengo  yao muhimu maishani. Sekta ya ICT inajenga fursa nyingi za ajira kwa vijana ambao wanatamani kutumia vipaji na ujuzi wao  ili kuleta mabadiliko chanya katika maisha yao.”

Na vile vile natoa pongezi za dhati kwa vijana waioweza kungia katika sita bora na kuweza kwenda kutuwakilisha nchini Ethiopia. Kwa hivi tulivyoviona tunamatumaini makubwa sana kwao na tunaamini watatuwakilisha vizuri katika mashindano hayo, aliongezea Mashiba.

 Airtel kupitia huduma zake za jamii, imeweza kuwafikia vijana zaidi ya 3600 kwa mwaka huu kwa kuwapatia vitendea kazi na mafunzo mbali mbali ya biashara kupitia mpango wake wa Airtel Fursa ,ambapo lengo ni kuwafikia vijana wengi zaidi hapa nchini.

No comments: