Tangazo

November 23, 2015

BIMA YA AFYA NHIF YAKANUSHA KUDAIWA NA HOSPITAL YA RUFAA MBEYA




Na Mwandishi wetu, 
Dar es salaam

 Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya nchini umekanusha kuwepo kwa madai yaliyotolewa na Hospital ya Rufaa  Mkoani Mbeya kuwa  wanaudai Mfuko jumla ya shilingi bilioni 2 na kwamba wanaudai Mfuko kutoka mwezi Juni, 2015.

Akizungumza jijini Dar es salaam Kaimu Mkurugenzi Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya  Ndugu Michael Mhando amesema madai yaliyotolewa na Hospital hiyo ya Rufaa Mkoa wa Mbeya  hayana ukweli wowote nakwamba mfuko huo  unalipa madai baada ya mtoa huduma kuwasilisha kwenye Mfuko.

Amesema madai   ya mwisho ya Hospitali hiyo kulipwa ni ya mwezi Agosti, 2015. Madai ya mwezi Septemba, 2015 yamewasilishwa kwenye Mfuko tarehe 4/11/2015 ambayo mpaka sasa yana siku 15 tu. Kwa hiyo Hospitali ya Rufaa ya Mbeya tumewalipa madai yao yote na kwa mwaka huu wa 2015 kuanzia Januari hadi Agosti 2015 tumewalipa kiasi cha shilingi bilioni 4.3.

Madai mengi ambayo yamekuwa yakiwasilishwa kwao yamegubikwa na udanganyifu mkubwa hali inayowafanya kuchukua muda mrefu katika uhakiki wake ikiwemo kuwapigia simu wagonjwa waliopewa huduma za matibabu.

Aidha Mhando amesema mfuko huo unatoa onyo kali kwa watoa huduma ambao wamekuwa bado wakijihusisha na udanganyifu wa aina yoyote kwa kuwa haitawaonea haya kuwafutia usajili na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.

Amesema Mfuko pia unazidi kutoa rai kwa watoa huduma kutumia fursa zinazotolewa na Mfuko katika kuhakikisha huduma za matibabu zinaboreshwa kwa wanachama na Watanzania kwa ujumla.
 
Wakati huo Kaimu mkurugenzi huyo amesema Katika kipindi hiki, baadhi ya watoa huduma wamekuwa wakitoa sababu mbalimbali za kushindwa kutoa huduma nzuri ama za kuridhisha kwa wanachama wao  na wananchi kwa ujumla kwa kisingizio cha kukosa fedha hali inayosababisha kukosa dawa, kukosa vifaa tiba na vitendanishi pamoja na kushindwa kuboresha mazingira ya vituo.

Watoa huduma hao wanadai hayo ama wanatoa visingizio vya kukwama huduma katika maeneo yao kutokana na NHIF kuchelewa kulipa fedha fedha za madai ambayo wametibia wanachama wake.
Amesema taarifa  hizo zinajenga mazingira kuwa NHIF ni kikwazo katika ufanisi wa vituo hivyo jambo ambalo si la kweli na limebeba taswira ya kuleta chuki baina ya wanachama ama wananchi na chombo chao ambacho kina dhamana ya kuwatibia.

Hata hivyo Mhando amekanusha kuwa wao  ndio kikwazo ama sababisho la huduma mbovu katika vituo hivyo nah ii inatokana na ukweli kwamba zipo jitihada mbalimbali ambazo NHIF imekuwa ikizifanya kuhakikisha inasaidiana na Serikali katika kuboresha huduma za vituo hivyo ili wananchi kwa pamoja wapate huduma zinazostahili.

(Imeandaliwa na Mtandao wa www.Jamiimoja.blogspot.com-0759406070)

No comments: