Tangazo

July 3, 2015

AIRTEL YAKABIDHI FUTARI KWA WATOTO YATIMA KATIKA VITUO VITATU MKOANI DAR

Meneja wa huduma kwa jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kulia), akiongea na wawakilishi wa vituo vitatu vya watoto yatima baada ya kukakabidhi msaada wa vyakula mbalimbali vya mfungo wa Ramadhani kwa wawakilishi wa vituo vya kulelea watoto waliokatika mazingira magumu. Vituo vilivyopata msaada huo ni pamoja na  Almadina cha Tandale, Dogodogo cha Kigogo na Hisani cha Mbaga wakishuhudiwa na baadhi ya watoto waishio katika vituo hivyo, katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Airtel kupitia mpango wake wa huduma kwa jamii imeanza kutoa futari kwa vituo mbali mbali hapa nchini.
Meneja wa huduma kwa jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kulia), akimkabidhi  bibi Kurudhumu Yusuph Juma mlezi wa kituo cha watoto yatima cha Al- Madina (wa pili Kulia) msaada wa vyakula mbalimbali kwa ajili ya mfungo  wa Ramadhani wakishuhudiwa na walezi wa vituo vingine vya Dogodogo kilichopo Kigogo  bw, Ditufu Ally (tatu Kulia) na Kituo cha Hisani kilichopo Mbaga bw. Twaha Kambaya (kushoto)  katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Airtel kupitia mpango wake wa huduma kwa jamii imeanza kutoa futari kwa vituo mbali mbali hapa nchini.
Meneja wa huduma kwa jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kulia), akimkabidhi  bw. Twaha Kambaya  (kushoto)   mlezi wa kituo cha watoto yatima cha Hisani kilichopo Mbagala msaada wa vyakula mbalimbali kwa ajili ya  mfungo huu wa Ramadhani wakishuhudiwa na baadhi ya watoto wa vituo hivyo na mlezi wa kituo cha Al- Madina bi  Kurudhumu Yusuph Juma (kati) katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Meneja wa huduma kwa jamii wa Airtel, Hawa Bayumi akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto waishio katika vituo vya kulelea watoto walio katika mazingira magumu wakati wa hafla ya kuwakabithi msaada wa vyakula kwaajili ya mfungo wa Ramadhani iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana, vituo vilivyopata msaada ni pamoja na  Almadina cha Tandale, Dogodogo cha Kigogo na Hisani cha Mbagala Dar es salaam.

No comments: