Tangazo

June 8, 2018

SERIKALI YASHAURIWA KUJENGA MAHABUSU ZA WATOTO KWENYE MIKOA NA WILAYA HAPA NCHINI




 Mratibu wa Chama cha Wanasheria Wanawake Mkoani Tanga Latiba Ayoub akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo ya siku moja iliyokuwa na lengo la kujaribu kujadili changamoto kwenye sheria za mtoto na kanunuzi zake hususani waliopo kwenye ukinzani nazo wakiwemo kama wadau iliyofanyika mjini hapa
  Mwanasheria wa Chama cha Wanasheria Wanawake Mkoani Tanga (Tawla) Mwanaidi Kombo akizungumza wakati wa warsha hiyo ya siku moja iliyofanyika ukumbi wa YDCP Jijini Tanga
Afisa wa Dawati Jeshi la Magereza mkoani Tanga ASP Halima Mswagilla akichangia jambo kwenye warsha hiyo
Wakili wa Serikali Rebbeca Msalangi akisisistiza jambo kwenye warsha hiyo wakati akiwasilisha mada

 Wakifuatilia hoja mbalimbali za wajumbe wa warsha hiyo
 Sehemu ya washiriki wakiendelea kufuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa
  Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwang’ombe Jijini Tanga Husna Abdi wa pili kutoka kulia akichukua baadhi ya dondoo kwenye warsha hiyo

SERIKALI imeshauriwa kujenga mahabusu za watoto kwenye mikoa na wilaya hapa nchini ili kuwaweka watoto waliokuwa katika ukinzani wa kisheria ambao wamekuwa wakifanya vitendo viovu.

Hatua hiyo itakuwa sehemu ya kuwaweka watoto happy wakiwa wanasubiri kesi zao kusikilizwa badala ya ilivyokuwa hivi sasa watoto hao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali kutokana na uhaba uliopo.

Hayo yalisemwa juzi na Mratibu wa Chama cha Wanasheria wanawake mkoani Tanga (TAWLA) Latifa Ayoub wakati wa warsha ya siku moja iliyokuwa na lengo la kujaribu kujadili changamoto kwenye sheria za mtoto na kanunuzi zake hususani waliopo kwenye ukinzani nazo wakiwemo kama wadau iliyofanyika mjini hapa

Alisema kutokana na uhaba wa mahabusu za watoto wamekuwa wakati mwengine wakikumbana na changamoto kadhaa wakati wakisubiri utaratibu wa kusikilizwa kesi zao wanazokabiliana nazo kabla ya kutolewa hukumu.

“Hivi sasa kuna watoto wanakuwa kuzidi umri wao na wanafanya vitendo viovu huku wazazi wakiwa hawana uwezo hivyo kupelekea wimbi lao kuwa wengi na mahabusu yao ni chache hivyo kuna umuhimu wa serikali kuliangalia jambo hili kwa mapana kwa kuziongeza angalau mkoa na wilaya “Alisema

Hata hivyo alisema pia sehemu hizo ambazo watakuwa wakiwekwa watoto hao itakuwa ni eneo ambalo watakaa wale ambao wapo kwenye ukinzani wa kisheria wakisubiri hitimisho la kesi zao ambazo wanatuhumiwa kuhusika nazo.

Naye kwa upande wake Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwang’ombe Jijini Tanga Husna Abdi alisema watoto wanaokinzana na sheria wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kuchanganywa na watu wazima watoto kutokupewa haki zao.

Alisema kupitia warsha hiyo ambayo wamekutana wadau mbalimbali wakiwemo ustawi wa Jamii,Jeshi la Polisi,Mahakamani wawe chachu ya kuielimisha jamii kuhusu haki zao ili kuhakikisha haki inatendeka vema kwa mujibu wa sheria.(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

June 6, 2018

Itazame Simulizi mpya iliyopewa jina la ‘Kinyago’

Kwa  nafasi ya upendeleo New Talents tunachukua fursa hii kukupa nafasi ya kwanza kuitazama hii video ya Simulizi mpya iliyo beba ujumbe mkubwa unaotakiwa kuwafikia Wanadamu, kwani Dunia inamambo mengi  ndio maana wengi wanajikatia tamaa kwa kuikosa thamani yao hapa Duniani.

Amini na kwambia Dunia bila changamoto haiwezi kunoga, ndio maana kila kukicha tumekuwa tukikutana na changamoto za hapa na pale kama vifo,ajali na manyanyaso.

 New Talents Tanzania Crew tunakuletea Simulizi ambayo imepewa jina la ‘KINYAGO’ Simulizi hii imegusa pande nyingi  katika maisha ya wanadamu, imeandikwa na Mrembo Rose Peter Maarufu kwa jina la ‘PUKUU’ chini ya usimamizi wa Director Mr.Super News  tunaomba Support yako katika kuufikisha ujumbe uliyomo ndani ya Simulizi hii kwa jamii Asante. 

KAMPUNI YA REGUS YAFUNGUA KITUO KIPYA CHA BIASHARA DAR ES SALAAM

Kampuni ya kimataifa ya Regus, ambayo inajihusisha na kupangisha ofisi za kisasa za muda na za kudumu imefungua kituo kipya cha nne cha ofisi za kupangisha jijini Dar es Salaam. 

 Jengo jipya la ofisi za Regus kwa ajili ya matumizi ya kupangisha ofisi zisizo na usumbufu wa masharti liko eneo la Msasani Penisula, na linazo ukubwa wa mita za mraba 590 kwa ajili ya matumizi ya ofisi za kisasa. 

 “Tumefungua jengo la nne la kituo cha biashara lenye maeneo ya ofisi za kupangisha,hii ni fursa pekee kwa Mashirika Yasio ya Kiserikali,na makampuni ya kimataifa kujipatia sehemu za ofisi za kisasa. Eneo hili la biashara limelenga makundi yote ikiwemo wajasiriamali wanaoanza biashara kwa kuwa bei zake za pango ni za kawaida na rahisi kuzimudu” alisema Joanne Bushell, Meneja wa Regus nchini. 

 Regus imepanua huduma zake kutokana na ongezeko la mahitaji ya ofisi kwa matumizi mbalimbali na kwa gharama nafuu bila kuhangaika kununua samani za ofisi, kuingia mikataba ya kipindi cha muda mrefu na kulipia huduma mbalimbali za matumizi ya ofisi kama umeme na maji.

 Kituo hicho cha biashara cha Regus kinazo ofisi za kupangisha, kumbi za mikutano zenye huduma mbalimbali ikiwemo mawasiliano ya uhakika kupitia mtandao wa internet na simu za mezani, majiko na sehemu za kupumzikia, huduma za usafi, huduma za mapokezi na utawala. Kampuni inao mpango wa kuendelea vituo vingine vya biashara katika siku za usoni kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya ofisi zisizo na masharti na usumbufu, Regus inaendesha vituo vya biashara katika miji ipatayo 900 kwenye nchi zaidi ya 120 duniani,ikiwa inahudumia wajasiariamali wa kawaida, watu binafsi na makampuni makubwa ya kimataifa.

June 5, 2018

WALINZI WA WANYAMAPORI WATAKIWA KUWA MAKINI NA WAADILLIFU


Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori nchini (TAWA), Meja Jenerali  mstaafu Hamisi Semfuko (wa pili kushoto mwenye miwani), akizungumza na walinzi wa wanyamapori katika maeneo yanayozunguka Pori ya Akiba la Maswa mkoani Simiyu alipokua akikagua shughuli za uhifadhi na ulinzi katika maeneo hayo juzi.
Xxxxxxxxxxxx

MARA

WALINZI wa wanyamapori katika maeneo yanayozunguka Pori ya Akiba la Maswa yanayopakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wametakiwa kuwa makini na waadilifu kutokana na kuongezeka kwa wanyama adimu wanaofika maeneo yao.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori nchini (TAWA) Meja Jenerali  mstaafu Hamisi Semfuko alipokua akikagua shughuli za uhifadhi na ulinzi katika maeneo hayo.

Meja Jenerali Semfuko, alisema kazi ya kupambana na ujangili inahitaji uvumilivu, uadilifu na ujasiri mkubwa kutokana na mazingira hatarishi yaliyopo.

"La muhimu kuna taatifa maeneo haya wameanza kuja wanyama adimu hivyo ningependa muongeze jitihada hizi mara dufu wanyama hao wasidhurike," alisema.

Katika ziara hiyo wajumbe wa Bodi ya TAWA walipokea taarifa ya timu ya pamoja kati ya TAWA, Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), Frankfurt Zoological Society  ( FZS), TAWIRI na Friedkin Conservation Fund (FCF) katika kuhifadhi na kulinda na kuhifadhi wanyama adimu.

Taarifa hiyo iliyowasilishwa na wataalamu Philbert Ngoti wa TANAPA na Gerald Nyaffi wa FZS katika  eneo la kitalu kilichopo Maswa Mbono kinachoendeshwa na kampuni ya Tanzania Game    Tracker Safaris  (TGTS).

Wataalam hao walisema wamefanikiwa katika mradi huo kwa ufadhili wa familia ya Friedkin inayomiliki TGTS ililiyofadhili fedha, vifaa pamoja na helikopta, kazi ijayotarajiwa kuendelea katika maeneo mengine.

Katika ziara hiyo TAWA  imeridhishwa na utendaji wa Makampuni ya uwindaji na upigaji picha za kitalii, yaliyopo katika maeneo yake kwa kusimamia uhifadhi na ulinzi pamoja na kuchangia miradi ya maendeleo ya wananchi yenye thamani zaidi ya sh 40 bilioni.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Usimamizi wa Wanyamapori nchini (TAWA), Dk James Wakibara akizungumza na waandishi wa habari juu ya mchango kwa jamii, uhifadhi na kiuchumi wa  makampuni ya uwindaji wa kitalii zilizowekeza katika maeneo yao.

Maeneo yaliyotembelewa na TAWA ni pamoja  na Hifadhi ya Jamii ya Wanyamapori(WMA) ya Makao wilayani Meatu inayosimamiwa na kampuni ya Mwiba Holdings Limited.

Dk Wakibara alisema, licha  mchango wa makampuni kwenye jamii, pia TAWA kupitia malipo  ya kampuni hizo, imekuwa ikitoa  takriban sh 6.5 bilioni kila mwaka kwa vijiji vyenye wawekezaji hao na halmashauri.

Makampuni hayo yamewekeza katika baadhi ya maeneo ya vitalu 159   vilivyopo nchini na maeneo ya hifadhi za jamii za wanyamapori (WMA) 38 zilizopo nchini.

"Hizi kampuni za kitalii zina mchango mkubwa sana pia katika uhifadhi wa maeneo haya, hasa katika vita dhidi ya ujangili ikizingatiwa asilimia 95 ya maeneo yaliyohifadhiwa nchini yapo chini ya TAWA"alisema

Alisema kwa sasa mapato ya TAWA kutokana na shughuli za uhifadhi, yamefikia dola milioni 20 lakini kuna mikakati ya kuongeza mapato hayo mara nne zaidi hadi kufikia dola milioni 80.


"kuna dhana potofu kuwa uwindaji wa kitalii ni kumaliza wanyama hili sio kweli, kwani haya makampuni hayajawahi kufikia hata robo  kiwango cha kuwinda wanyama ambacho kinatolewa kila mwaka na TAWA na mashirika ya kimataifa"alisema

Mwenyekiti wa bodi ya TAWA, Meja Jenerali  mstaafu Hamisi Semfuko alisema mamlaka hiyo ipo katika mabadiliko  makubwa ili kuhakikisha jamii inanufaika zaidi ya uhifadhi wa wanyamapori,katika kusaidia miradi ya kijamii ya maji, afya Elimu na uhifadhi.

Mwenyekiti huyo na bodi yake ambao walitembelea pori la Makao, lilipo mpakani mwa Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro na Meatu,alisema wameridhishwa na utendaji wa kampuni ya Mwiba Holding katika eneo hilo.

KIGWANGALLA AAGIZA MSAKO MKALI KWA WALIOUA SIMBA TISA SERENGETI

 Baadhi ya simba kati ya tisa waliouwawa kikatili kwa kulishwa sumu, kukatwa na kuchomolewa baadhi ya viungo vyao na wananchi katika kijiji cha Nyichoka, wilaya ya Serengeti mkoani Mara.

Na Hamza Temba-Dodoma
............................................................
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameagiza Kikosi Kazi Dhidi ya Ujangili cha Taifa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Serengeti kuwasaka watu waliohusika na mauaji ya simba tisa katika kijiji cha Nyichoka, wilaya ya Serengeti mkoani Mara na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Dkt. Kigwangalla ametoa agizo hilo ofisini kwake Jijini Dodoma jana baada ya kupokea taarifa rasmi ya mauaji hayo ya kikatili yaliyoripotiwa hivi karibuni kwa simba hao kulishwa sumu kali katika kijiji hicho huku mmoja akikatwa miguu, mkia, ngozi ya juu ya mgongo na kuchukuliwa baadhi ya viungo vyake ambapo amesema mauaji hayo hayavumiliki kwa kuwa yana athari kubwa kiikolojia, kiutalii na uchumi wa Taifa kwa ujumla.

"Bahati mbaya sana ni kuwa anapouawa simba kwa sumu hafi peke yake, inakufa familia nzima ya simba, na mara nyingi wanakufa pia wanyamapori wengine wanaodowea nyama na wanaokula mizoga. Walipouawa simba wa Ruaha hivi karibuni walikufa fisi zaidi ya 70 na ndege mbeshi zaidi ya 100, achilia mbali wadudu," amesema Dkt. Kigwangalla kwa masikitiko makubwa.

Amesema pamoja na faida kubwa za simba kwa Taifa kiuchumi, Kijiji cha Nyichoka pekee walikouwawa simba hao ni katika sehemu iliyofaidika sana na miradi ya ujirani mwema kutoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

"Wanyama hawa jamii ya paka wakubwa ni muhimu sana kwa kuweka mizania ya ikolojia sawa, maana wanadhibiti idadi ya wanyama wala nyasi kwa kuwala, bila hivyo hifadhi zote zinaweza kugeuka kuwa jangwa. 

"Hakuna mtalii atakayekuja hifadhini asitamani kumuangalia simba, mfalme wa pori. Wanapouawa maana yake tunashusha hadhi ya hifadhi zetu kiutalii na hivyo kutishia kupoteza mapato yanayotokana na utalii" amesisitiza Dkt. Kigwangalla. 

Amesema tukio hilo la kuuwawa kwa Simba wa Ikolojia ya Serengeti sio la kwanza kutokea hapa nchini ambapo mwishoni mwa mwaka jana simba wengine watano waliuawa pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha. 

"Mwaka huo huo mwanzoni simba watatu nao walipigwa risasi kikatili wilayani Serengeti huku mwaka 2015 simba 7 wakauwawa tena kwa sumu, huko huko Serengeti".

Akizungumzia sababu za ujangili huo amesema mara nyingi ni kwa ajili ya kulipiza kisasi baada ya ng’ombe wa wananchi kuliwa na simba, changamoto ambayo husababishwa na wananchi wenyewe kusogelea na kuweka makazi karibu kabisa na mipaka ya hifadhi za wanyamapori kwa lengo la kulisha mifugo pembezoni na wakati mwingine ndani ya hifadhi hizo kinyemela.

Simba ambao wanakadiriwa kuwa zaidi kidogo ya 22,000, pamoja na wanyama wengine jamii ya paka wamepungua sana miaka ya hivi karibuni kiasi cha kuwekewa tishio la kutoweka hapa duniani. Duma nao wanakadiriwa kubaki 1,200 pekee.
 Askari wa wanyamapori wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakikusanya miili ya simba  tisa waliouwawa kikatili kwa kulishwa sumu, kukatwa na kuchomolewa baadhi ya viungo vyao na wananchi katika kijiji cha Nyichoka, wilaya ya Serengeti mkoani Mara  hivi karibuni kwa ajili ya kuwafanyia uchunguzi kubaini chanzo cha vifo vyao.
 Askari wa wanyamapori wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakikusanya miili ya simba  tisa waliouwawa kikatili kwa kulishwa sumu, kukatwa na kuchomolewa baadhi ya viungo vyao na wananchi katika kijiji cha Nyichoka, wilaya ya Serengeti mkoani Mara  hivi karibuni kwa ajili ya kuwafanyia uchunguzi kubaini chanzo cha vifo vyao.

June 4, 2018

UMEME NI NISHATI MBADALA ILIYO NAFUU KWA MATUMIZI YA NYUMBANI: KAMOTE

 Bw. Ally M. Koyya, (kulia), kutoka idara ya Masoko TANESCO, akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea kwenye banda la Shirika hilo kwenye maonesho ya Nishati Mbadala yanayokwenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam Juni 4, 2018.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

SHIRIKA la Umeme Nchini (TANESCO) limesema hakuna sababu yoyote kwa wananchi kuogopa kutumia nishati ya umeme kwa matumizi mbalimbali ya nyumbani kwani ni nafuu mno ukilinganisha na nishati nyingine.
Afisa Mazingira wa Shirika hilo, Bw.Yusuf Kamote, amesema hayo kwenye maonesho ya Nishati mbadala ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani yanayoendelea kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Juni 4, 2018, ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Mkaa ni ghali tutumie Nishati mbadala”.
“Siku zote tunasema umeme wa TANESCO ni umeme wa bei nafuu, jambo la msingi ambalo wananchi wanapaswa kuelewa ni matumizi sahihi ya vifaa vya umeme kulingana na mahitaji.” Alisema.
Alisema kwa mfano mtu anatumia kifaa kinachohitaji WATI 100 (100watts) kwa saa moja lakini anatumia kifaa cha WATI 200 (200Watts) kwa saa na kwa mahitaji yanayofanana, bila shaka hayo sio matumizi bora ya umeme.
Bw. Kamote pia alishauri, wananchi wanapotaka kununua vifaa vya umeme, wanapaswa kukague kiasi cha umeme kinachohitajika kwenye kifaa husika anachotaka kununua na vifaa hivyo hupimwa kwa kutumia WATI (Watt ).
“Ukitumia pasi ya umeme ya WATI 1000 (1000Watts), kwa saa moja ni sawa na kutumia Unit 1 ya umeme kwa hivyo hakuna sababu ya kununua pasi ya umeme ya WATI2000 (2000Watts), kwa matumizi ya kawaida kwani pasi ya aina hiyo kwa matumizi sawa na ile ya WATI1000, matumizi yake yataongezeka, kutoka unit 1 hadi uniti 2.” Alifafannua.
Akieleza zaidi Bw. Kamote hakuna sababu tena ya kutumia mkaa kama nishati ya kupikia kwani hivi sasa yapo majiko ya umeme ambayo yanasaidia kudhibiti matumizi yaumeme yasiyo sahihi kwani.
“Kinachohitajika mpishi unatakiwa kuandaa vyakula unavyotaka kupika kabla ya kuwasha jiko lako la umeme, vyakula vikiwa tayari hapo ndipo unatakiwa kuwasha jiko lako tayari kwa kupika.” Alisema na kuongeza
Maonesho hayoyakliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais,  yalizinduliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wiki iliyopita na yanatariwa kufungwa na Rais John Magufuli, Jumanne Juni 5, 2018.

 Wanafunzi wa shule ya sekondari Kanosa ya jijini Dar es Salaam, wakipatiwa maelezo ya kitaalamu na wataalamu wa TANESCO (Kushoto).
Afisa Mazingira wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Bw. Yusuf Kamote, (kulia), akimsikiliza Afisa Uhusiano wa Shirika hilo, Bi. Samia Chande.


 Wanafunzi wa shule ya sekondari Kanosa ya jijini Dar es Salaam, wakipatiwa maelezo ya kitaalamu kuhusu matumizi bora ya nishati ya umeme walipotembelea banda la Shirika hilo leo Juni 4, 2018.
 Bw. Ally M. Koyya, (kulia), kutoka idara ya Masoko TANESCO, akimsikiliza mwananchi huyu aliyefika kwenye banda la Shirika hilo kupata elimu ya umeme.

WATANZANIA WATAKIWA KUJIUNGA NA MPANGO WA BIMA YA AFYA





 Daktari wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) Dennis David akimpima mkazi wa Jiji la Tanga Octaviani Moshiru kwenye banda lao lililopo kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga kunakoendelea maonyesho ya sita ya biashara ya kimataifa
  Daktari wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) Dennis David akimpima mkazi wa Jiji la Tanga Octaviani Moshiru kushoto akimsikiliza kwa umakini mkazi wa Jiji la Tanga
 Daktari wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) Lawi Kupaza akimpa ushauri mkazi wa Jiji la Tanga mara baada ya kupima afya.
Katibu tawala mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi akipima afya
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Hillary Ngonyani akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) lililopo kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga kunakofanyika Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Jumanne Shauri kulia ni Afisa Matekelezo wa Mfuko huo Macrina Clemens anayefuata ni Afisa Masoko na Elimu kwa Umma Makao Makuu Hawa Duguza
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Jumanne Shauri kushoto akisaini kitabu cha wageni kulia ni Afisa Matekelezo wa Mfuko huo Macrina Clemens anayefuata ni Afisa Masoko na Elimu kwa Umma Makao Makuu Hawa Duguza
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Jumanne Shauri kushoto akizungumza na maafisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mkoani Tanga kulia ni Afisa Matekelezo wa Mfuko huo Macrina Clemens anayefuata kushoto ni Afisa Masoko na Elimu kwa Umma Makao Makuu Hawa Duguza
 Afisa Matekelezo wa Mfuko huo Macrina Clemens kulia akisisitiza jambo kwa wananchi waliofika kwenye banda lao kupata elimu ya mpango wa kujiunga na bima ya Afya
 Katibu Tawala wa mkoa wa Tanga (RAS) Mhandisi Zena Saidi akiwa na tisheti akijiandaa kuwapa watoto zawadi wakati alipotembelea banda hilo kushoto Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu
sehemu ya watoto waliojiunga na mpango wa Toto Afya kadi

NA MWANDISHI WETU, TANGA.

WATANZANIA wametakiwa kujiunga na mpango wa bima a Afya ili waweze kunufaika na huduma za matibabu ya uhakika wakati wanapokuwa wakiugua na hivyo kuwapunguzia mzigo wa kuingia gharama kubwa.

Hayo yalisemwa leo na Afisa Masoko na Elimu kwa Umma wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya (NHIF) Makao Makuu Hawa Duguza wakati akizungumza kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga kunakoendelea maonyesho ya biashara ya kimataifa.

Licha ya mfuko huo kutoa elimu juu ya umuhimu wa mpango wa bima lakini pia wanaendelea kutoa huduma za upimaji wa afya na kutoa ushauri kwa wananchi ambao wamekuwa wakifika kwenye banda lao lililopo kwenye maonyesha hayo.

Alisema mpango wa bima ni mzuri kutokana na kuwapa uhakika wa matibabu wakati wanapokuwa wakikumbana na maradhi mbalimbali na hivyo ni muhimu kujiunga nao ili waweze kuona manufaa makubwa wanayoweza kuyapata.

Aidha pia aliwahamasisha kujiunga na mpango wa kikoa na toto Afya kadi ambazo ni muhimu kwa ajili ya kuweza kupata huduma nzuri kipindi ambacho wanapatwa na changamoto za kuugua hususani watoto wadogo wakati wa ukuaji wao.

“Ndugu zangu maradhi huwezi kujua yanakuja lini hasa kwa watoto wadogo wakati wa ukuaji wao hivyo niwasihi muone njia nzuri ya kuwawekea akiba ya matibabu kwa kuwaingiza kwenye mpango huu wa toto afya kadi kwani hii ni kumuhakikisha mtoto wako huduma wakati wote wanapougua”Alisema.

Alisema pia jamii haiwezi kupata maendeleo ikiwa watakuwa hawana afya bora hivyo ni muhimu kuendelea kuhamasishana kujiunga na mpango huo kwa lengo la kuweza kunufaika na huduma za matibabu (habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

June 1, 2018

TBL GROUP YAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUPANDA MITI MKOANI KILIMANJARO

 Wafanyakazi wakijiandaa kuanza zoezi la kupanda miti wilayani Siha, Kilimanjaro.
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL waliopo katika mafunzo ya kukuza vipaji wakishiriki zoezi la kupanda mito wilayani Siha, Kilimanjaro.
Wafanyakazi wakipanda miti wilayani Siha, Kilimanjaro.
Meneja Masoko na Udhamini wa TBL Group, George Kavishe akiongea wakati wa tukio la upandaji miti Baadhi ya wananchi wakifuatilia hotuba wakati wa hafla hiyo

May 31, 2018

MAFURIKO SAME YAKATA MAWASILIANO YA MIOUNDO MBINU ,WANACHI WATUMIA MITUMBWI NA TREKTA KUSAFIRISHA MALI ZAO.

Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro,Aisha Amour (aliyenyoosha mkono) akiwa na baadhi ya Wajumbe wa kamati ya Maafa  ya mkoa wakiwa eneo la Ruvu Darajani ambako magari yanaishia baada ya miuondo mbinu ya barabara kujaa maji .
Moja ya barabara ambayo ilikuwa ikitumiwa na wakazi wa maeneo ya Ruvu Muungano na Darajani ikiwa imejaa maji na kusababisha adha kwa wasafiri.
Baadhi ya wananchi wakijaribu kuyahama makazi yao baada ya nyumba zao kuzingirwa na maji katika Vijiji vya Ruvu  Marwa na  Ruvu Mferejini.
Baadhi ya wananchi wamekuwa wakitumia usafiri wa pikipiki kwa maeneo ambayo bado hayajafikwa na maji mengi.
Kutokana na miundombinu ya barabara kuharibika vibaya baadhi ya wafanyabiashara ya bidhaa ndogondogo wametumia kadhia hiyo kununua bidhaa kama Unga na Mchele na kuwauzia wananchi waliozingirwa na maji kwa bei ya juu.
Usafiri pekee kwa sasa katika maeneo hayo ni Trekta na Mitumbwi ambayo imekuwa ikitumika kuhamisha mali pamoja na wananchi.
Na Hii ndio hali Halisi ya wananchi katika maeneo hayo wamelazimka kutumia mitumbwi kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine .

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.